Monday 22 June 2015

BENKI YA NBC, TAWI LA SINGIDA YASAIDIA MASHUKA 30, KWA HOSPITALI YA MKOA WA SINGIDA.

MKUU wa Wilaya ya Singida, Saidi Amanzi (kulia), akikabidhi moja ya shuka kwa mganga mfawidhi, hospitali ya mkoa Singida,Dk.Ramadhani Kabala,kati ya mashuka 30 @ 15,000/=, baada ya mkuu wa wilaya huyo kupokea kutoka kwa meneja wa benki ya NBC Tawi la Singida, Japheth Mazumira, ili kupunguza uhaba wa mashuka na magodoro, kwenye hospitali hiyo.
KAIMU afisa Muuguzi mkuu, hospitali ya Mkoa wa Singida, Teresia Ntui (kushoto, mganga mfawidhi na watumishi wengine wa hospitali hiyo, wakifurahia pamoja, muda mfupi baada ya kupokea msaada wa mashuka 30, kutoka kwa benki ya NBC, Tawi la Singida.
MENEJA benki ya NBC, Tawi la Singida, Japheth Mazumira (kushoto), akikabidhi shuka kwa mkuu wa wilaya Singida, Saidi Amanzi, kwa ajili ya kukabiliana na upungufu wa mashuka na magodoro katika hospitali hiyo. Wengine wanaoshuhudia ni wataalamu wa afya katika hospitali hiyo.
BAADHI ya wanawake waliojifungua wodi ya sita, katika hospitali hiyo,wakiwa wamekaa watatu kwenye kitanda kimoja, huku wameshikilia watoto wao, kutokana na uhaba mkubwa wa mashuka na magodoro.
Na Elisante John, Singida Juni 22, 2015. HOSPITALI ya Mkoa wa Singida inakabiliwa na upungufu mkubwa wa mashuka zidi ya 2,000 na magodoro 230, hali inayoathiri utoaji huduma ya afya na uzazi kwa wagonjwa na wajawazito wanaokwenda kupata tiba kwa afya na uzazi. Mkuu wa wilaya ya Singida, Saidi Amanzi, Mganga mafawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Ramadhani Kabala na kaimu afisa muuguzi mkuu, Teresia Ntui, wametoa wito kwa wadau mbalimbali kusaidia vifaa mbalimbali, ikiwemo mashuka na magodoro, ili kuboresha hudumza ya afya. Ili kukabiliana na changamoto hizo, benki ya NBC, Tawi la Singida, imetoa msaada wa mashuka 30, kwa ajili ya kupunguza kero wanazokumbana nazo wagonjwa, katika hospitali hiyo. Hospitali ya Mkoa wa Singida iliyojengwa mwaka 1954, ina jumla ya vitanda 300, lakini hivi sasa serikali ya Mkoa inaendelea na ujenzi wa hospitali kubwa ya rufaa, katika eneo la Mandewa, manispaa ya Singida.

Monday 18 May 2015

MBUNGE VITI MAALUMU (CCM) MKOA WA SINGIDA ATOA MSAADA KWA JUMUIYA YA UWT NA VIKUNDI VYA VIJANA

Na Elisante John, Singida Mei 18, 2015. IKIWA imebakia miezi mitano, kabla ya Tanzania kufanya uchaguzi mkuu, Wanawake wametakiwa kujenga tabia ya kupendana na kuonyana kwa upendo, ili kupata viongozi bora. Hayo yameelezwa na mbunge viti maalumu Mkoa wa Singida, na mjumbe kamati ya siasa mkoa wa Singida, Martha Mlata, alipokuwa akiongea na wanawake wa Wilaya ya Mkalama, Iramba, Ikungi na Singida Mjini, waliokutana, ili kujitathimini, kabla ya uchaguzi mkuu, utakaofanyika Oktoba, mwaka huu. Licha na tathimini hiyo, Mlata pia alitoa msaada wa pikipiki saba kwa ajili ya jumuiya ya UWT Wilaya ya Mkalama, Iramba, Singida mjini, Singida vijijini na Ikungi, pia alikabidhi baiskeli kwa ajili ya makatibu kata UWT, katika kata zote za mkoa wa Singida. Pia alikabidhi pikipiki moja na jezi jozi nne kwa ajili ya kikundi cha vijana, kilichopo kwenye kijiji cha Ibaga, wilaya ya Mkalama.