Monday 18 May 2015

MBUNGE VITI MAALUMU (CCM) MKOA WA SINGIDA ATOA MSAADA KWA JUMUIYA YA UWT NA VIKUNDI VYA VIJANA

Na Elisante John, Singida Mei 18, 2015. IKIWA imebakia miezi mitano, kabla ya Tanzania kufanya uchaguzi mkuu, Wanawake wametakiwa kujenga tabia ya kupendana na kuonyana kwa upendo, ili kupata viongozi bora. Hayo yameelezwa na mbunge viti maalumu Mkoa wa Singida, na mjumbe kamati ya siasa mkoa wa Singida, Martha Mlata, alipokuwa akiongea na wanawake wa Wilaya ya Mkalama, Iramba, Ikungi na Singida Mjini, waliokutana, ili kujitathimini, kabla ya uchaguzi mkuu, utakaofanyika Oktoba, mwaka huu. Licha na tathimini hiyo, Mlata pia alitoa msaada wa pikipiki saba kwa ajili ya jumuiya ya UWT Wilaya ya Mkalama, Iramba, Singida mjini, Singida vijijini na Ikungi, pia alikabidhi baiskeli kwa ajili ya makatibu kata UWT, katika kata zote za mkoa wa Singida. Pia alikabidhi pikipiki moja na jezi jozi nne kwa ajili ya kikundi cha vijana, kilichopo kwenye kijiji cha Ibaga, wilaya ya Mkalama.