Sunday 7 December 2014

BENKI YA NMB, TAWI LA SINGIDA IMESHEREHEKEA SIKU YA KUJUMUIKA NA WAFANYAKAZI WOTE, 'NMB FAMILY DAY', KWA AMANI, NA KUFANA KWA KIWANGO KIKUBWA, HUKU WAFANYAKAZI WAKE WAKILA, KUNYWA NA KUFURAHIA KUPITIA MICHEZO MBALIMBALI

SHEREHE KWA WAFANYAKAZI WA BENKI YA NMB, TAWI LA SINGIDA JINSI ZILIVYOFANA KATIKA VIWANJA VYA HOTELI YA KBH, ILIYOPO ZIWA SINGIDANI.
BENKI ya NMB, Tawi la Singida imefanya sherehe kubwa kwa ajili ya siku ya wafanyakazi wake, ‘NMB Family’, iliyofanyika katika hotel ya KBH mjini Singida na kufana kwa kiwango kikubwa. Licha ya familia hizo kukutana pamoja, pia yalifanyika mashindano mbalimbali, ikiwemo kufukuza kuku (wanaume na wanawake), mpira wa miguu (wanaume) na muziki (dansi) kwa watoto. Hata hivyo watoto wawili wa mtumishi wa benki hiyo, Bw. Joseph, walifanikiwa kushinda baada ya kusakata vyema muziki wa kizazi kipya na kupewa zawadi mbalimbali na meneja wa tawi hilo, Bibi.Christine Mwangomo. MWISHO

No comments:

Post a Comment