Sunday 7 December 2014

MBUNGE VITI MAALUMU (CCM) MKOA WA SINGIDA, MARTHA MLATA AMEISAIDIA SEKONDARI YA NDUGUTI SH.MILIONI TATU KUONDOA TATIZO LA MAJI SHULENI HAPO

MBUNGE viti maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Mlata ametoa msaada wa shilingi milioni tatu kwa sekondari ya kata ya Nduguti, wilaya ya Mkalama mkoani Singida, kwa ajili kuodoa tatizo la maji linaloikabili shule hiyo kwa muda mrefu sasa. Alilazimika kutoa kiasi hicho, baada ya kusomwa risala kwenye mahafali ya sita ya shule hiyo, kwamba inakabiliwa na changamoto nyingi, mojawapo ikiwa ni tatizo la maji, ambalo husababisha wanafunzi kupoteza muda mwingi kusaka maji, badala ya kushiriki masomo. Hata hivyo Mlata aliitaka halmashauri ya wilaya ya Mkalama kuhakikisha nayo inachangia kiasi cha fedha kitakachopungua, ili kazi ya kuvuta maji kwa kutumia mtandao wa bomba iweze kukamilika haraka, na yeye akabidhiwe mapema januari mwakani wakati shule zitakapofunguliwa. Licha ya kutoa kiasi hicho cha fedha, Mlata alikabidhi pia mipira na jezi za mchezo wa soka, kwa ajili ya wasichana na wavulana wa shule hiyo, msaada uliogharimu zaidi ya Sh.laki mbili na nusu. MWISHO.

No comments:

Post a Comment