Thursday 7 November 2013

MAMLAKA YA MAPATO (TRA) MKOA SINGIDA YAZINDUA SIKU YA MLIPA KODI...

Elisante John MAMLAKA ya mapato (TRA) Mkoa wa Singida unatarajia kuongeza mapato yake mara mbili ya kiwango cha makusanyo ya kodi, kutoka Sh. Bilioni 4.1 mwaka huu na kufikia zaidi ya Sh. Bilioni 8.3 ifikapo mwaka 2017/18. Afisa elimu kwa mlipa kodi wa malaka hiyo Mkoa wa Singida, Zacharia Gwagilo alisema hayo, wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya saba, siku ya mlipa kodi kimkoa katika ofisi za TRA, mjini Singida. Alisema katika kusherehekea siku ya mlipa kodi TRA Singida inaadhimisha kwa kusaidia wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya Manyoni na Iramba, kutembelea kituo cha wasioona Sabasaba, kusaidia kituo cha watoto wenye ulemavu wa akili Siuyu na kufanya semina kwa makundi mbalimbali ya walipa kodi. Kwa mujibu wa Gwagilo, ujumbe wa siku ya mlipa kodi mwaka huu ni “TULIPE KODI KWA MATOKEO MAKUBWA SASA”.

No comments:

Post a Comment