Sunday 23 March 2014

JUMUIYA YA SERIKALI ZA MITAA (ALAT) na nchi ya CANADA ZAENDESHA MAFUNZO SINGIDA

KATIKA picha baadhi ya washiriki wa mafunzo wakisikiza kwa makini hotuba ya ufunguzi wa mafunzo uliofanywa na mkuu wa Wilaya Singida Mwalimu Queen Mlozi kwa ajili ya wataalamu wa halmashauri za wilaya, wenyeviti wa halmashauri na mameya wa Manispaa wa kanda ya kati (Singida, Tabora, Dodoma na Kigoma), yaliyofanyika ukumbi wa halmashauri Wilaya Singida, kwa ajili ya kuwaongezea uwezo wa kufanya kazi kwa weledi zaidi. Na Elisante John, Singida March 23, 2014:JUMUIYA ya Serikali za Mitaa (ALAT) kwa kushirikiana na serikali ya Canada, inaendesha mafunzo kwa wataalamu wa halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji nchini ili kuwaongezea uwezo waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi. Hayo yalibainishwa juzi na Armstrong Amani,mratibu wa taifa mpango wa MPED, unaofadhili mafunzo hayo ambayo tayari yametolewa katika mikoa ya kanda ya ziwa, mashariki, kaskazini na sasa Mkoani Singida kwa kushirikisha mikoa ya Kigoma, Tabora, Dodoma na Singida. Armstrong alisema kuwa baada ya wataalamu wa halmashauri kupata mafunzo hayo, wataongeza ufanisi kazini kulingana na ubunifu watakaogundua kutokana na elimu wanayopatiwa kupitia mpango huo wa Municipal Partnership for Economic Development (MPED). Mapema akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya Singida Mwalimu Queen Mlozi aliwataka wataalamu hao kuhakikisha wanazingatia vyema mafunzo wanayofundishwa, ili baadaye siku za usoni yawasaidie kuwaleleta wananchi maendeleo. “Ninawaomba sana muwe makini muda wote wakati mnafundishwa…mkirudi lazima mkalete mabadiliko katika wilaya zenu ili wananchi wapate maendeleo kama vile ilivyokusudiwa na serikali,”alisema Mlozi. Aidha mwezeshaji wa mafunzo hayo Amosi Migire, ambaye pia ni mratibu kiongozi mpango wa MPED Mkoa Morogoro alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kubwa ya maendeleo katika halmashauri za wilaya nchini kutokana na kutumia dira na vipaombele vilivyowekwa kwenye maeneo husika. Kwa mujibu wa Amstrong, mpango wa Municipal Partnership for Economic Development duniani upo nchi za Tanzania, Bukinafaso, Mali, Cambodia, Nicaragua, Vietinam na Bolvia, huku katika bara kla Afrika ukihusisha nchi tatu pekee. Hapa nchini MPED unatoa mafunzo kwa maofisa maendeleo ya jamii, mipango, fedha, ushirika, maofisa biashara, madiwani (mwenyekiti au meya) na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya. MAELEZO YA PICHA YA KWANZA-IMG 1387:Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya MPED kwa ajili ya kujengea uwemo, wakiwemo wataalamu,Wenyeviti na mameya wa halmashauri za wilaya na manispaa wa mikoa ya Kigoma, Tabora, Dodoma na Singida, yanayotolewa mjini Singida chini ya usimamizi wa mamlaka za serikali za mitaa nchini (ALAT) inayoshirikiana na nchi ya Canada. MAELEZO YA PICHA YA PILI IMG 1892:Mkuu wa Wilaya Singida Mwl. Queen Mlozi akifungua mafunzo hayo. PICHA na Elisante John-Singida. MWISHO.

No comments:

Post a Comment