Sunday 30 March 2014

SHULE YA SEKONDARI UNYAHATI HAINA CHOO WALA MADAWATI.

BAADHI ya wanafunzi wa shule ya sekondari Unyahati iliyopo tarafa ya Ikungi Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wakitumia viti vya plastiki kukalia na mapaja kukandamizia daftari wakati wa kuandika. Pia kwenye picha kinaonekana choo cha shimo kikiwa kimezungushiwa majani ya mimea jambo ambalo ni hata wakati wa masika, kwa mujibu wa mwalimu Mboya David wa shule hiyo shimo la choo hicho hutitia wakati wa mvua za masika na kulazimika kuchimba kingine wmajira ya kiangazi. Picha nyingine ikionyesha ofisi ya mkuu wa shule, ambacho kimetokana na moja ya darasa kutumika kama ofisi, hiyo yote imetokana na jamii inayozunguka shule hiyo kukataa kuchangia miradi ya maendeleo wakidai kuwa serikali inazo fedha za kutosha.
Na Elisante John, Ikungi March 30, 2014. SHULE ya sekondari Unyahati iliyopo wilaya ya Ikungi Mkoani Singida inakabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo uhaba wa vyoo hali inayohatarisha afya kwa wanafunzi wanaolazimika kutumia choo cha nyasi. Kaimu mkuu wa shule hiyo Mboya David alisema kutokana na wazazi au walezi kutochangia miradi ya maaendeleo ikiwemo ile ya sekta ya elimu, walimu na wanafunzi wa shule hiyo walilazimika kuchimba choo hicho ambacho hata hivyo wakati wa masika hutumbukia ardhini. "Hapa kijijini ukizungumza juu ya michango!, wazazi na walezi hawatakuelewa, wameelezwa na viongozi wao kuwa serikali inazo fedha nyingi kwa jili ya kugharamia miradi yote…Wananchi hawahusiki kabisa na shughuli za kuchangia fedha,’alisema mwalimu huyo. Kufuatia kero hiyo, mwalimu David ameiomba serikali kuniusuru shule hiyo kwa kutenga fedha kwa ajili ya kukabiliana na kero mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vyoo jambo ambalo ni muhimu sana kiafya. David alizitaja changamoto nyingine shuleni hapo ni wanafunzi wa kidato cha kwanza kutumia viti vya plastiki darasani, hali inayosababisha waweze kuandika wakiwa wanatumia mapaja yao kama meza. Changamoto nyingine shuleni hapo ni kukosekana kwa nyumba za walimu na kusababisha walimu kutembea kilomita nane kwenda na kurudi shuleni hai makao makuu ya Wilaya, mjini Ikungi walikopanga. "Jengo la utawala tunalotumia limetokana na kubadili matumizi ya vyumba viwili vya madarasa… tunakabiliwa na upungufu mkumbwa wa samani ikiwemo makabati kitendo kinachotulazimisha kutumia viti vya plasitiki kuhifadhia nyaraka mbalimbali,"alisema mwalimu David. Kuhusu vyumba vitatu vya maabara,David alisema kuwa hali ni mbaya mno kwa sababu hata kutenga eneo lenyewe la kujenga vyumba hivyo,halijatengwa. MWISHO.

No comments:

Post a Comment