Sunday 23 March 2014

MAKADA CCM WAIOMBA SERIKALI KUWADHIBITI WANASIASA WANAOZUIA JAMII KUCHANGIA MIRADI YA MAENDELEO

Picha mbalimbali zikionnyesha sherehe ya kuwaapisha Makamanda wapya wa CCM kutoka kata 26 za Wilaya Ikungi katika sherehe zilizofanyika Kijiji cha Makiungu, kata ya Mungaa mheni rasmi akiwa ni Mkuu wa Wilaya hiyo Manju Msambya.
Elisante John, Singida March 23, 2014. SERIKALI imeombwa kutumia nguvu ili kuwadhibiti wanasiasa wanaokwamisha Wananchi kuchangia fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye maeneo yao, hasa ile inayohusiana na sekta ya elimu. Hayo yamebainishwa na makada 26 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM0 walioapishwa na Mkuu wa Wilaya Ikungi mkoani Singida Manju Msambya kuwa makamanda wa chama hicho ngazi ya kata. Mmoja wa makada wa chama hicho Celestne Yunde alisema miradi mingi ya kijamii kwenye maeneo yanayoshikiliwa na vyama vya upinzani wilayani humo hivi sasa yapo nyuma kimaendeleo kutokana na viongozi wa vyama vya upinzani kuwakataza wananchi kuchangia fedha za miradi. Kutokana nna hali hiyo Yunde ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Ikungi (CCM) aliiomba serikali kuwadhibiti wanasiasa wa aina hiyo, ili kuharakisha maendeleo kwenye maeneo hayo. Aidha Sanka Pius Sanka na alhaji Haji Mukhandi kutoka jimbo la Singida Mashariki walitoa wito kwa jamii kutowachagua tena wanasiasa wa aina hiyo wakati wa uchaguzi mkuu ujao, kutokana na kukwamisha maendeleo katika maeneo wanayoongoza. Walisema kuwa miaka mitano iliyopita jimbo hilo lilipiga hatua kubwa kwa ujenzi wa shule za sekondari baada ya kila kata kufanikisha zoezi hilo, lakini miaka minne baadaye ari ya jamii kuchangia maendeleo imeshuka, kiasi cha kusababisha kuwa jimbo la mwisho Singida katika ujenzi wa vyumba vya maabara. “Kuingia madarakani kunahitaji mbinu nyingi ili kuwashahwishi wananchi wakuchague kama wanavyofanya wanasiasa uchwara…wananchi sasa wamejifunza katika miaka hii minne, naamini hawatafanya kosa tena la kumchagua mtu anayewafaa kuwasaidia kuleta maendeleo,”alisema Sanka Pius. Kwa upande wake mgeni rasmi wakati wa kuwaapisha makamanda wapya wa CCM, Wilaya Ikungi Mkuu wa Wilaya hiyo Manju Msambya alisema kuwa kabla hajashughulikiwa na Serikali katika kutekeleza ujenzi wa vyumba vya maabara, atahakikisha anawashughulikia kwanza watu hao ili kukomesha tabia hiyo. “Ninachoweza kusema kwa watu kama hawa…mimi nilikula kiapo mbele ya mkuu wangu wa kazi mkuu wa mkoa, sitakubali kushughulikiwa kwa uzembe wa kushindwa kukamilisha ujenzi wa maabara, nitahakikisha nawashughulikia kwanza wote wanaokwamisha kazi hii,”alisema Mkuu huyo wa wilaya. Kwa mujibu wa Msambya, Wilaya hiyo ina jumla ya shule za sekondari 28, lakini hadi sasa maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya maabra ni dhaifu kwa asilimia 18 mpaka 65, huku wilaya hiyo ikishika nafasi ya mwisho, wakati muda uliowekwa na Mkoa kukamilisha kazi hiyo ni juni 30 mwaka huu. Kwa mujibu wa Msambya wilaya zinazoongoza kwa ujenzi wa maabara mkoani Singida ni halmashauri ya wilaya Mkalama na Iramba. MWISHO.

No comments:

Post a Comment