Monday 24 March 2014

MKUTANO MKUU WA SINGIDA PRESS CLUB WAFANYIKA MANYONI KWA AMANI NA KUPATA KATIBU MTENDAJI MPYA.

VIONGOZI wa juu wa Klabu ya wanahabari Mkoa wa Singida, Mwenyekiti Seif Takaza (katikati), kushoto ni katibu msaidizi Emmanuel Michael na Damiano Mkumbo-Makamu mwenyekiti wakati wa mkutano mkuu uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (Maktaba) mjini Manyoni.
SEHEMU ya wajumbe wa kamati ya utendaji Hudson Kazonta (kushoto) akiwa na mjumbe mwenzake wakifuatilia kwa makini maendeleo ya mkutano huo. Na Elisante John, Manyoni March 24,2014. KLABU ya wanahabari Mkoa wa Singida imefanya uchaguzi mdogo na kumchagua mwanachama wake Pascal Tantau awe katibu mtendaji wa Singpress ili kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Abby Nkungu aliyejiuzulu disemba 30 mwaka jana kwa madai ya kuzorota afya yake. Katika mkutano mkuu huo wa mwaka uliofanyika kwa amani na utulivu Wilayani Manyoni, Pascal ambaye ni mwandishi wa kujitegemea gazeti la Raiatanzania, Tanzania daima na kituo cha Redio WAPO jijini Dar es Salaam, alipata kura 15 za ndio, mbili za hapana na kura moja iliharibika. Kutokana na uchaguzi huo mdogo uliofanyika wakati wa mkutano mkuu wa mwaka, Pascal atakuwa madarakani kwa mwaka mmoja hadi mwaka 2015 utakapofanyika uchaguzi wa viongozi wote ili kuendana sawa na mwongozo wa katiba ya Umoja wa klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC). Akishukuru baada ya kuchaguliwa, Pascal aliwashukuru wanachama wote kwa kumwamini na kumpatia madaraka hayo makubwa na akaahidi kutumia nguvu, akili na uwezo wake wote kuisaidia klabu ili iweze kupiga hatua kubwa ya maendeleo. Kwa upande wake mwenyekiti wa klabu hiyo Seif Takaza aliwashukuru wanachama wote kwa kufanikisha kazi hiyo na akaongeza kuwa hii inaonyesha jinsi gani sasa klabu ilivyokomaa kutokana na wanachama pia uongozi bora chini ya usimamizi wa kamati ya utendaji ya Singpress. Uchaguzi huo ulilazimika kufanyika kufuatia aliyekuwa katibu wake Abby Nkungu kujiuzulu kwa madai kuwa ameagizwa na daktari wake anayeishi Nairobi nchini Kenya kwamba asifanye kazi inayomlazimu kutumia akili nyingi, kutokana na upasuaji wa jicho aliofanyiwa miaka mitano iliyopita. MWISHO.

No comments:

Post a Comment