Sunday 23 March 2014

WAUMINI WA KANISA LA WANDIVENTISTA (WASABATO) WAJITOLEA DAMU

Singida March 23, 2014. WAUMINI wa madhehebu mbalimbali ya dini na jamii kwa ujumla wametakiwa kujenga utamaduni wa kuchangia damu, ili kurahisisha upatikanaji wa damu salama kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa waliolazwa hospitalini. wanaohitaji waliolazwa hospitalini kutokana na kusumbuliwa na maradhi mbalimbali, ikiwemo pia wanaopatwa na ajali. Rai hiyo imtolewa na waumini wa kanisa la Waadiventista-WASABATO, lililopo Unyankindi mjini Singida, wakati wanachangia damu, chini ya usimamizi wa chama cha Msalaba mwekundu, Mkoa wa Singida. Walisema licha ya kuwasaidia wagonjwa wanaoteseka hospitalini kwa kupungukiwa damu, zoezi hilo pia linazidisha upendo miongoni mwao. Aidha Mkurugenzi wa vijana kutoka kanisa hilo Eliphasi Nkuka alisema upungufu wa damu uliopo katika hospitali nyingi nchini utakwisha na maisha ya wagonjwa wanaokabiliwa na tatizo hilo yataokolewa iwapo kutakuwa na akiba ya kutosha kwenye benki ya damu salama nchini. “Kazi hii ya kumponya binadamu ilianzishwa na Yesu mwenyewe…sisi tumeamua kujitolea kutoa damu ili kuwaokoa wenzetu wanaoteseka hospitalini kwa magonjwa mbalimbali na ajali..,”alisema mkurugenzi wa vijana katika kanisa hilo Eliphas Nguka. Zoezi hilo ililotanguliwa na msaada kwa wagonjwa waliolazwa hospitali ya Mkoa wa Singida mwingine uliopelekwa kituo cha watoto yatima Upendo kilichopo Manguamitogho Manispaa Singida , uligharimu zaidi ya Sh. 800,000. Naye mratibu wa Mkoa, mpango wa taifa damu salama Sostenes Ndyetabura aliitaka jamii kuiga mfano wa waumini wa kanisa la Wasabato ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa damu lililopo katika akiba ya benki ya damu salama, ambayo kwa mkoa wa Singida, ipo Mkoani Tabora. Aidha muuguzi wa zamu wodi ya watoto hospitali ya Mkoa wa Singida Marieta Bayo kwa niaba ya watoto waliolazwa, alishukuru kwa msaada huo na kuomba msaada zaidi kutoka kwa wote wenye uchungu na watoto wanaoteseka hospitalini kutokana na maradhi mbalimbali. MWISHO.

No comments:

Post a Comment