Sunday 11 May 2014

MBUNGE WA SINGIDA MASHARIKI TUNDU LISSU AKIWA AMEFUATANA NA MBUNGE WA ARUSHA MJINI GODBLESS LEMA AFANYA MKUTANO IKUNGI NA KUVALISHWA MGOLOLE NA KUPEWA MKUKI IKIWA NI ISHARA YA MTU SHUJAA.

WANANCHI wa Ikungi, Jimbo la Singida Mashariki wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Tundu Lissu alipozungumza na Wananchi hao kwenye mkutano wa hadhara kuzungumzia mambo mbalimbali ikiwemo kuwashaishi vijana na wanawake kujiandika kwenye daftari la kudumu la kupigia kura.
TUNDU Lissu akiwa juu nya jukwaa kuwahutubia wananchi waliojitokeza kusikiliza hotuba yake aliyoitoa makao makuu ya wilaya Ikungi.
. AKILAKIWA na wananchi baada ya kuvikwa vazi la mgolole na kupewa ngao na mkuki ikiwa ni ishara ya mtu shujaa.
Singida Mei 12, 2014. MBUNGE wa Singida Mashariki Tundu Lissu amehimiza vijana, wanawake na walemavu kuzikabili changamoto zilizopo jimboni mwake kwa kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kudumu la kupigia kura na kuwania nafasi balimbali za uongozi, ili watatue kero hizo wakiwa madarakani. Akizungumza na wananchi wa Ikungi Mjini, Mbunge huyo aliyeingia madarakani kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kwa tiketi ya CHADEMA, Lissu alisema kuwa sasa umefika wakati kwa makundi hayo kuwania uongozi, badala ya kuwaachia watu wachache kujirudia kila chaguzi. “Ndugu zangu, hasa vijana na wanawake muda ukifika wa kujiandikisha hakikisheni mnatumia vizuri nafasi hii…tusione aibu kugombea nafasi hizi, tukishinda vizuri nafasi ya vitongoji, vijiji na mitaa itaturahisishia pia kushinda uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na Rais hapo mwakani,”alisema Lissu. Aidha Lissu aliyechaguliwa mwishoni mwa wiki iliyopita na kiongozi wa kambi ya upinzani Freeman Mbowe kuwa waziri kivuli, wizara ya katiba na sheria (muungano), alisema wajumbe wa bunge la katiba kutoka upinzani hawatarudi kujadili muswada wa katiba, hadi hapo lugha chafu za matusi zitakapokoma bungeni. Mapema kwenye mkutano huo mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema aliyefuatana na Lissu, aliwaeleza wananchi waliokusanyika makao makuu ya Wilaya ya Ikungi kuendelea kumpa ushirikiano mbunge wa jimbo hilo, ili aendelee kuwapigania. “Mbunge wenu ni mbunge wa taifa, mpeni nafasi afanye kazi ya kuwakomboa watanzania…akienda sehemu mbalimbali za nchi akasimama na kuzungumza, wananchi watamsikiliza na kumuelewa kwa sababu ni mtu wa watu, mpeni nafasi afanye kazi ya kuwatetea wananchi,”alisema. Katika ziara hiyo, Lissu alipokewa na wananchi wa jimbo lake katika kijiji cha Ulyampiti wilaya Ikungi akitokea bungeni Dodoma, na kuvishwa mgolole na akina mama kisha wazee wanaume wakamkabidhi ngao na mkuki, ikiwa ni ishara ya mtu shujaa. MWISHO.

No comments:

Post a Comment