Sunday 29 September 2013

WIKI YA NENDA KWA USALAMA ILIVYOKUWA SINGIDA JUMAPILI...

MRATIBU wa mamlaka ya usafiri nchi kavu na majini (SUMATRA) Mkoa Singida Bw. Daniel Chilongani akihutubia wananchi na wadau wa usafirishaji, katika sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya stendi ya Msufini jana katika kuadhimisha WIKI YA NENDA KWA USALAMA kimkoa zilizofanyika jana jumapili. KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Singida Geofrey Kamwela akizungmza na wananchi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika sherehe za WIKI YA NENDA KWA USALAMA Kimkoa zilizofanyika viwanja vya stendi ya Msufini mjini Singida. MMOJA wa askari akitoa maelekezo ya alama za barabarani mbele ya mgeni rasmi Daniel Chilongani ambaye ni mratibu wa SUMATRA Mkoa, katika sherehe za WIKI YA NENDA KWA USALAMA zilizofanyika kwenye viwanja vya stendi ya Msufini mjini Singida (wa pili kulia) ni kamanda wa polisi mkoani Singida, Geofrey Kamwela.

No comments:

Post a Comment