Tuesday 1 October 2013

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi (CCM) Manispaa Singida Janeth Nyakonji akimkaribisha mgeni rasmi mjumbe wa halmashauri kuu NEC-CCM taifa Singida mjini Hassan Mazala kufungua semina ya mafunzo kwa viongozi wa jumuiya hiyo.Kulia ni MNEC CCM Singida mjini Bw. Mazala. Mjumbe wa NEC-CCM Wilaya Singida mjini Hassan Mazala akifungua semina ya mafunzo ya siku mbili inayohudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa jumuiya ya wazazi wilaya Singida mjini. Wa kwanza kushoto na mjumbe wa halmashauri ya CCM Singida mjini Duda Mughenyi na anayefuata ni mwenyekiti jumuiya ya wazazi Bi. Janeth Nyakonji. Baadhi ya viongozi wa jumuiya ya wazazi (CCM) manispaa ya Singida wanaohudhuria semina hiyo kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi (FDC), mjini Singida.

No comments:

Post a Comment