Wednesday 16 October 2013

MWENYEKITI CCM MKOA SINGIDA MGANA MSINDAI AZINDUA TAWI LA HAILA KIJIJI CHA URUGHU WILAYANI IRAMBA...

MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai Oktoba 16,2013 amefanya ziara katika kijiji cha Urughu Wilaya Iramba na kuzindua tawi jipya lililopo kitongoji cha Haila lenye wananchama zaidi ya 300 na baadaye kufanya mkutano eneo la makao makuu ya kata (Urughu), kabla ya mkutano huo wa hadhara ambapo wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali, mapema alikagua ujenzi wa vyumba vitatu vya maabara sekondari ya Urughu na kukagua ujenzi wa kituo cha afya kinachojengwa kwa nguvu za wananchi wa kata hiyo na kuridhishwa sana na maendeleo ya ujenzi huo. Hata hivyo aliwasihi wananchi wa kata hiyo kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo ili kuharakisha maendeleo kwenye eneo lao.

No comments:

Post a Comment