Saturday 19 October 2013

MAHAFALI YA TANO SHULE YA SEKONDARI KATA YA MWARU YAMEFANYIKA LEO SHULENI HAPO

SHULE ya kata Sekondari ya Mwaru iliyopo tarafa ya Sepuka Wilaya Ikungi imefanyika leo shuleni hapo ikitanguliwa na mgeni rasmi katika mahafali hayo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Mgana Msindai kuwakabidhi vyeti wanafunzi 11 wanaofanya mtihani mwaka huu kuhitimu kidato cha nne.


 
MMOJA wa wanafunzi wa Sekondari ya Mwaru iliyopo tarafa ya Sepuka Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida akipokea cheti kwa mgeni rasmi Mgana Msind Mwenyekiti wa CCM Mki ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoani humo, katika sherehe za mahafali ya tano shuleni hapo leo. PICHA nyingine juu inawaonyesha wanafunzi kidato cha nne wakicheza muziki wa hiphop maarufu kwa jina la ‘Muziki wa kizazi kipya’ kama ishara ya kufurahia kumaliza miaka mine salama.


 SEHEMU ya madarasa ya shule ya Sekondari Mwaru iliyopo tarafa ya Sepuka Wilaya Ikungi Mkoani Singida.

BAADHI ya wazazi na walezi waliohudhuria sherehe hizo.

Thursday 17 October 2013

KAMBI YA UVCCM SINGIDA VIJIJINI ILIVYOFANA WAKATI WA UFUNGAJI ULIOFANYIKA KTK KATA YA KINYETO....

BAADHI ya vijana kutoka UVCCM Singida vijijini wakiwa ndani ya ukumbi katika makao makuu ya kata ya Kinyeto, tayari kumsikiliza mgeni rasmi Mwenyekiti wa CCM mkoa Singida Mgana Msindai (hayupo pichani). Ufungaji rasmi wa kambi hiyo umefanyika leo Oktoba 17,2013.
VIONGOZI mbalimbali wa CCM wakiwemo Makamanda wa UVCCM wa kata zote za Wilaya Singida Vijijini (waliovaa majoho) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Singida Mgana Msindai, wan ne kutoka kushoto waliosimama, kabla ya kufunga kambi ya vijana iliyoendeshwa kwa siku saba kwenye kata ya Kinyeto. SEHEMU ya vijana, wake kwa waume wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi akifunga kambi hilo la siku saba, lililofanyika kijiji, kata ya Kinyeto Singida Vijijini.

KAMBI YA UVCCM SINGIDA VIJIJINI ILIYOFANYIKA KWA SIKU SABA KATIKA KATA KINYETO YAFUNGWA...

KUTOKA kulia,mtu wa pili ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa Wwa Singida, Mgana Msindai akiwa meza kuu kabla ya kufunga kambi ya wiki moja ili kufundwa juu ya mada mbalimbali, yaliyoandaliwa na Umoja wa Vijana CCM Singida Vijijini. Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa CCM Wilayani humo Narumba Hanje na kulia kwa Msindai ni Mwenyekiti wa UVCCM Singida vijijini Shabani Mang’ola.

Wednesday 16 October 2013

MWENYEKITI CCM MKOA SINGIDA MGANA MSINDAI AZINDUA TAWI LA HAILA KIJIJI CHA URUGHU WILAYANI IRAMBA...

MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai Oktoba 16,2013 amefanya ziara katika kijiji cha Urughu Wilaya Iramba na kuzindua tawi jipya lililopo kitongoji cha Haila lenye wananchama zaidi ya 300 na baadaye kufanya mkutano eneo la makao makuu ya kata (Urughu), kabla ya mkutano huo wa hadhara ambapo wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali, mapema alikagua ujenzi wa vyumba vitatu vya maabara sekondari ya Urughu na kukagua ujenzi wa kituo cha afya kinachojengwa kwa nguvu za wananchi wa kata hiyo na kuridhishwa sana na maendeleo ya ujenzi huo. Hata hivyo aliwasihi wananchi wa kata hiyo kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo ili kuharakisha maendeleo kwenye eneo lao.

Wednesday 9 October 2013

WAANDISHI WA HABARI 20 KUTOKA SINGIDA, TABORA, DODOMA NA KIGOMA WAPEWA MAFUNZO JUU YA KUANDIKA HABARI ZA UKATILI DHIDI YA BINADAMU

MKUU wa Wilaya Bahi na Kaimu Mkuu wa Mkoa Dodoma, Betty Mkwasa akiwa na Deodatus Balile mkufunzi wa mafunzo kwa waandishi 20 wa habari juu ya kuandika kwa ufasaha taarifa za Ukatili wa kijinsia dhidi ya binadamu yaliyofanyika katika hotel ya Fifty six Mjini Dodoma. Hapa ni baada ya kuwa amefungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Dk. Rehema Nchimbi. WAANDISHI wa habari 20 kutoka mikoa ya Kigoma, Tabora, Singida na Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na kaimu mkuu wa mkoa Dodoma Betty Mkwasa (katikati waliokaa kwenye viti), kulia ni mkufunzi wa mafunzo hayo Jamila na kushoto ni Balile.

Sunday 6 October 2013

SHEREHE ZA UWT ZILIVYOFANA WILAYA SINGIDA

SHEREHE ZA UWT WILAYA SINGIDA VIJIJINI ZILIVYOFANA NA KUHUDHURIWA NA MAELFU YA AKINA MAMA KUTOKA KONA ZOTE ZA WILAYA HIYO, AMBAZO ZILIHUTUBIWA NA MBUNGE WA JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI LAZARO NYALANDU AMBAYE PIA NI NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII.

Tuesday 1 October 2013

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi (CCM) Manispaa Singida Janeth Nyakonji akimkaribisha mgeni rasmi mjumbe wa halmashauri kuu NEC-CCM taifa Singida mjini Hassan Mazala kufungua semina ya mafunzo kwa viongozi wa jumuiya hiyo.Kulia ni MNEC CCM Singida mjini Bw. Mazala. Mjumbe wa NEC-CCM Wilaya Singida mjini Hassan Mazala akifungua semina ya mafunzo ya siku mbili inayohudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa jumuiya ya wazazi wilaya Singida mjini. Wa kwanza kushoto na mjumbe wa halmashauri ya CCM Singida mjini Duda Mughenyi na anayefuata ni mwenyekiti jumuiya ya wazazi Bi. Janeth Nyakonji. Baadhi ya viongozi wa jumuiya ya wazazi (CCM) manispaa ya Singida wanaohudhuria semina hiyo kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi (FDC), mjini Singida.