Tuesday 15 April 2014

MRADI WA UMEME UNAOTUMIA NGUVU YA UPEPO KUGHARIMU ZAIDI YA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 285 SINGIDA.

NAIBU waziri wa nishati na mdini Stephen Maselle (kushoto) akisaini kitabu cha wageni katika eneo la uwezekezaji nishati ya umeme unaotumia nguvu ya jua unaotarajiwa kujengwa kwenye eneo la Kisaki chini ya kampuni ya Wind East unaofadhiliwa na nchi ya United Kingdom (UK), kulia kwake ni waziri wa nishati na mabadiliko ya hali ya hewa wa UK Gregory Barker, balozi wa UK hapa nchini Dianna Melrose, mkuu wa Mkoa Singida Dk. Prseko Kone (wa mwisho kushoto).
Wakiwa eneo la mradi lenye mkondo wa upepo mkali kwa ajili ya kuzalisha umeme unaotumia nguvu ya upepo. Na Elisante John, Singida Aprili, 2014. SERIKALI ya Uingereza imeiomba Tanzania kuharakisha mchakato wa kuharakisha ujenzi wa kuzalisha umeme unaotumia nguvu ya upepo Mkoani Singida, ambao utahifadhi pia mazingira, ili kupunguza tatizo la nishati hiyo nchini. Waziri wa nchi, wizara ya nishati na mabadiliko ya hali ya hewa wa Uingereza Gregory Barker (Mbunge) amesema hayo, alipotembelea eneo la uwekezaji umeme wa upepo, katika eneo la Kisaki, Mjini Singida. Naye naibu waziri nishati na madini Stephen Masele amelikumbusha shirika la umeme nchini (TANESCO) kukamilisha haraka mazungumzo kati yao na mwekezaji wa mradi huo kampuni ya Wind East Africa inayotarajiwa kutumia dola za Kimarekani zaidi ya Milioni 285 hadi kukamilika. Aidha mhandisi wa mradi huo Baptiste Bargés alisema ingawa mchakato huo unasuasua kuanza, lakini utakapoanza utasaidia sana kuongeza uwezo wa TANESCO wakati utakapounganishwa kwenye gridi ya taifa, wakati Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Parseko Kone alieleza kufurahishwa na wananchi wa eneo la kisaki katika kuukubali mradi huo ambao utaongeza sana nishati hiyo nchini. Kwa mujibu wa naibu waziri Masele, jumla ya megawati 2,700 hadi 3,000 zinatarajiwa kuzalishwa hadi ifikapo mwaka 2015, wakati kwa sasa ni megawati 1,500 tu, ndizo zinazozalishwa nchini. MWISHO.

No comments:

Post a Comment