Tuesday 8 April 2014

KILIMO KINAWEZA KUWAKOMBOA VIJANA IWAPO WATAAMUA KUJISHUGHULISHA.

VIONGOZI wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dodoma wakiwa na viongozi wao wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa, wakikabidhi Pikipiki tano kwa wenzao wa Singida tayari kwa ajili ya kuendelea na mbio za uzalendo kitaifa, makabidhiano yaliyofanyika kijiji cha Lusilile Wilayani Manyoni.
k
NAIBU Katibu mkuu Jumuiya ya Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi Zanzibar Shaka Hamud Shaka (kulia aliyekingwa)akipeana mkono na mmiliki wa shamba la kampuni ya Singida agriculture Co Ltd Bw. Ali Mohammed lililopo kijiji cha Mkiwa Wilaya Ikungi aliyeajiri vijana zaidi ya 300 kwenye shamba hilo. Pia katika ziara hiyo naibu katibu mkuu aligawa kadi za UVCCM kwa vijana 300 wanaofanya kazi katika shamba hilo (mwenye kofia kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida Martin Lissu). PICHA nyingine inamwonyesha kijana akichapa kazi ya kuchambua maharage mabichi baada ya kuvuna, tayari kwa ajili ya kujaza kwenye kreti ili kusafirishwa nje ya nchi ikiwemo barani Ulaya. PICHA nyingine inaonyesha mmiliki wa shamba hilo Bw. Ali Mohammed (kulia)akimwomnyesha mgeni rasmi (katikati) naibu katibu mkuu Jumuiya ya UVCCM Shaka Humud Sshaka aliyefanya ziara shambani hapo akiwa na msafara wa pikipiki za uzalendo kitaifa, kushoto ni mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida Martin Lissu. Na Elisante John, Ikungi KILIMO hai ni moja ya kazi ambazo vijana wengi hawataki kufanya, lakini pamoja na fursa hii nzuri hali ni tofauti kwa wawekezaji wa nje ambao wamekuwa wananufaika kiuchumi kutokana na mazao bora wanayolima na kuvuana. Naibu katibu mkuu Jumuiya ya Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Zanzibar Shaka Hamdu Shaka alisema hayo kwenye msafara wa mbio za uzalendo za pikipiki kitaifa, alipokuwa anaongea na vijana wanaofanya kazi shambani mwa mwekezaji, Singida Agriculture Co Ltd, lililopo Mkiwa wilaya Ikungi. Naye meneja mkuu wa Singida Agriculture Co Ltd Ali Mohammed anasema wakulima wengi nchini bado wanakabiliwa changamoto nyingi katika kuboresha mazao yao, hali aliyodai kuwa wanayo kazi kubwa kuhakikisha wanakabiliana kikamilifu na matatizo hayo. Baadhi ya vijana wanaofanya kazi shambani humo akiwemo Anita Ramadhani,Jasmin Paulo na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida Martine Lisu, walieleza fursa mbalimbali kupitia kilimo na maeneo mengine, ambao walisema kuwa iwapo vijana watajikita katika kazi hizo ni wazi maisha yao yataboreka. Mbio za hizo za pikipiki kitaifa zilizinduliwa na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein Februari 22 mwaka huu, zikiwa na lengo la miaka 50 ya Muungano wa Tanzania, yenye kauli ‘Tanzania kwanza’. MWISHO.

No comments:

Post a Comment